Thursday 13 June 2013

R.I.P RAPPA LANGA: ALIFARIKI DUNIA JANA JION!!!!!!!!!


Msanii wa hiphop Tanzania, Langa Kileo a.k.a Langa amefariki dunia jana (13th) muda mfupi uliopita  katika hospitali ya muhimbili jijini Dar.Akizungmza na Clouds Fm, Afisa uhusiano wa hospitali ya taifa ya Muhimbili, Ameniel Aligaesha, amethibitisha kwamba msanii Langa, amefariki dunia leo hii saa kumi na moja za jioni, baada ya kufikishwa hospitalini hapo juzi jioni.
hata hivyo uongozi wa Muhimbili hauna uwezo wa kusema kilichomuua Langa, kutokana na maadili ya kazi zao, bali ndugu wa  marehem.
Kifo cha Langa kimetufika ikiwa ni siku 17 tu tangu kufariki kwa msanii mwingine wa hiphop na freestyle master Albert Mangwea A.k.a Ngwea.
Mungu ailaze roho ya matehem mahali pema peponi

No comments:

Post a Comment