Tuesday 28 May 2013

NEY WA MITEGO: ASILIMIA KUBWA YA WASANII WANAOOA AU KUOLEWA WANAFELI KIMUZIKI


Ikiwa ni miezi mitatu tu imebaki girlfriend wa Rapper Ney wa mitego "Siwema" kujifungua, Ney ameongea juu ya kushuka kwa mafanikio ya wasanii mara baada ya kuoa, ambapo yeye hatarajii kuoa hivi karibuni.
Ney amesema wengi wa wasanii bongo mara tu baada ya kuoa wanashuka kimziki na kuwataja majina kwa kuwatolea mfano ambapo amesema Marlow kapotea baada ya kuoa, Matonya, Z Anto na Shetta pia nyimbo zake kadhaa zimebuma baada ya kuoa.
"kuna ngoma yangu inaitwa "utakula jeuri yako", ambayo inaelezea vitu vyote hivyo, ambavyo may be watu hawavijui, aaah na pia inaonyesha unatakiwa kufanya nini ukiwa kwenye mazingira hayo, ya kwamba tayari umeshakuwa kwenye ndoa, wasanii wengi sana sio tanzania tu dunia nzima, ukioa au ukiolewa na game yako inaisha, otherwise unatakiwa kuwa mjanja sana, kama alivyokuwa mjanja Jay Z na Beyonce, zipo techniques ambazo unatakiwa kufanya, sio kukurupuka tu na kuoa, na ndio maana asilimia kubwa hasa kibongo bongo sisi wengi ambao wameoa wamefeli , kwa aslilimia nyingi sana wamefeli  ijapokuwa hili tatizo ni la dunia nzima."
"wapo wengi ndugu yangu Matonya alipotea, Z Anto alivyooa kapotea, Marlow alivyooa kapotea, Shetta kaoa juzi tu zimebuma kadhaa hapa katikati, nafikiri hii ni mifano hai ambayo ipo, so watu wanatakiwa kujipanga, so ukiskia mi nimeoa ujue nimejipanga, najua hatua mia zitakuja mbele, cause i know what am doing, hao waliooa wana nyimbo nyingi nzuri na zinatoka lakini zinakuwa hazikiki kama mwanzo walivyokuwa wakitoa nyimbo, sio kwamba wanakuwa hawarikodi wanarikodi , wimbo mzuri, na kiwango chako kinaweza kuwa hakijashuka, lakini mapokeo yanakuwa ni tofauti, na sio msanii tu hata wafanya biashara na watangazaji pia

No comments:

Post a Comment